• English
  • Kiswahili
  • Nini maana ya Bookrithyms | MuzikiRiwaya?

    Bookrithyms|MuzikiRiwaya ni mradi wa kisanaa unaounganisha fasihi andishi na muziki. Hapa, riwaya, mashairi na maandishi ya kifasihi kutoka kwa mwandishi “bingwa wa taharuki” Hussein Tuwa, hubadilishwa kuwa nyimbo — ambapo hadithi haziishii kuwa za kusomwa tu, bali pia za kusikika kimuziki. Maandishi yaliyozaliwa kwa wino yanapata mdundo. Kurasa zilizobeba maandishi, zinapata sauti. Kila wimbo ndani ya Bookrithyms huanzia kama kipande cha kazi ya fasihi asilia — sura ya riwaya, mstari wa ndani wa mhusika, au hisia iliyofichika kwenye simulizi. Muziki unakuwa njia ya kuendeleza hadithi, si kuibadilisha. Bookrithyms si tu muziki pekee, wala si tu fasihi andishi peke. Ni mahali ambapo tanzu hizi mbili za sanaa zinakutana na kuishi pamoja.
    hadithi zinaimba, na muziki unasimulia
    /wp-content/themes/artist-single-page/images/main.png
    Kutoka Ukurasa hadi Midundo

    Kutoka Ukurasa hadi Midundo

    ✍🏾

    Uandishi

    Riwaya na maandishi ya Hussein Tuwa

    📖

    Uchaguzi

    Mazingira & Hisia Zilizochaguliwa kwa Umakini

    🎼

    Tafsiri

    Maneno yaliyobadilishwa kuwa midundo

    🎤

    Utumbwizaji

    Muziki uliotolewa na ZHI VAGO, KOKKO RIKKOH, MTOTO SHOO

    WASANII WETU

    MuzikiRiwaya inatoa kazi za fasihi sauti ya muziki. Kila msanii hubadilisha hadithi za Hussein Tuwa kuwa midundo, melodi, na maonyesho.

    /wp-content/themes/artist-single-page/images/ZhiVago.png

    Zhi VAGO

    ZHI VAGO, sauti kuu ya muziki wa Riwaya.

    Mfahamu Zhi VAGO
    /wp-content/themes/artist-single-page/images/koko1.png

    Kokko Rikkoh

    KOKKO RIKKOH muelezea hadithi kwa njia ya muziki yenye nguvu.

    Mfahamu Kokko Rikkoh
    /wp-content/themes/artist-single-page/images/mtoto_shoo1.png

    MTOTO SHOO

    MTOTO SHOO anaongeza midundo ya hisia katika radha ya Riwaya.

    Mfahamu MTOTO SHOO